Hivi umewahi kujiuliza, hii michuano ya kombe la mabingwa ulaya maarufu kama ‘Uefa Champions League’ ilianza vipi? Kama hukuwahi kufuatilia, twende pamoja. Kwenye miaka ya 1950 huko, kulikuwa na kombe likiitwa ‘Latin Cup’ ambalo lilikuwa likizikutanisha klabu zilizotwaa ubingwa kutoka katika nchi nne pekee; Uhispania, Ureno, Ufaransa, na Italia.